Friday, September 23, 2016

WENGE APUUZA KITABU KIPYA CHA MOURINHO.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hatasoma kitabu ambacho meneja wa Manchester United Jose Mourinho amekaririwa akisema atapasua sura ya Mfaransa huyo. Mourinho amekuwa akikwazana mara kadhaa na Wenger wakati akiinoa Chelsea ambapo kuna wakati aliwahi kumuita mtaalamu wa kushindwa. Akihojiwa kuhusiana na kitabu hicho, Wenger amesema yeye anazungumza kuhusu soka na sio jambo lingine lolote na kwasasa anazingatia mchezo wao muhimu wa kesho dhidi ya Chelsea. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kamwe hayuko katika hali kubomoa bali kujenga na amekuwa akimheshimu kila mtu katika mchezo huo wa soka. Wenger amesema kauli iliyotolewa na Mourinho katika kitabu hicho haihusiani na masuala ya soka ndio maana hana mpango wa kushughulika nayo.

No comments:

Post a Comment