Friday, September 23, 2016

SPURS YAMUONGEZA MKATABA WALKER.

KLABU ya Tottenham Hotspurs, imetangaza kumsainisha mkataba mpya Kyle Walker ambao unatarajiwa kumalizika mwaka 2021. Mkataba wa sasa wa Walker ulikuwa umalizike Juni 2019, lakini klabu hiyo imemua kumuongeza mkataba mwingine kama ilivyofanya kwa nyota wengine wa kikosi cha kwanza akiwemo Christian Eriksen, Dele Alli, Eric Dier na Danny Rose. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, amekuwa akianza katika kikosi cha kwanza toka msimu wa 2011-2012 na ameisaidia Spurs kumaliza katika nafasi ya tatu chini ya meneja Mauricio Pochettino msimu uliopita. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Walker amesema ni heshima kubwa kwake na amemshukuru mwenyekiti pamoja na meneja kwa kuwa na imani naye.

No comments:

Post a Comment