Friday, October 21, 2016

FUCHS APEWA MKATABA MPYA LEICESTER.

KLABU ya Leicester City imetangaza kumpa mkataba mpya Christian Fuchs ambao utamuweka hao mpaka mwaka Juni 2019. Nyota huyo wa kimataifa wa Austria ameshacheza mechi 45 toka ajiunge na Leicester akiwa mchezaji huru kabla ya kuanza kwa msimu uliopita. Akihojiwa Fuchs amesema amefurahishwa kusaini mkataba huo kwani amekuwa na muda mzuri toka ajiunge na klabu hiyo. Fuchs sasa anaungana na nyota wengine wa klabu hiyo akiwemo Jamie Vardy, Riyad Mahrez, Wes Morgan na Kasper Schmeichel ambao pia tayari wameshasaini mikataba mipya.

No comments:

Post a Comment