Friday, October 21, 2016

LIVERPOOL KUMUWEKEA KIGINGI GOMEZ JANUARI.

KLABU ya Liverpool inadaiwa kuwa itazuia ofa yeyote ya mkopo kwa Joe Gomez katika usajili wa dirisha dogo Januari mwakani. Inaaminika kuwa Bournemouth wanataka kumchukua beki huyo kutoka kwa Liverpool kwa makubaliano ya muda mfupi. Mbali na Bournemouth lakini pia klabu ya Huddersfield Town inayoshiriki ligi ya ubingwa ambayo inanolewa na msaidizi wa zamani wa Jurgen Klopp katika klabu ya Borussia Dortmund, David Wagner nayo pia imetajwa kumtaka beki huyo. Hata hivyo, Liverpool wanaonekana kutokuwa na mpango na kumuacha beki huyo kwani wanataka kuanza kumrejesha taratibu katika kikosi cha kwanza baada ya kukaa nje ya uwanja kwa mwaka mmoja kufuatia kuumia goti.

No comments:

Post a Comment