Friday, October 21, 2016

POGBA ANAHITAJI MUDA - MOURINHO.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema Paul Pogba anahitaji muda ili kuonyesha uwezo wake Uingereza baada ya kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 4-1 waliopata dhidi ya Fenerbahce. Pogba aliyevunja rekodi ya usajili ya dunia kwa kunyakuliwa kwa kitita cha euro milioni 89 kutoka Juventus, alifunga bao moja kwa penati na lingine kwa shuti la mbali jana katika mchezo wa makundi wa Europa League uliofanyika Old Trafford. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 bado hajarejea katika kiwango chake toka arejee United baada ya kukaa Turin kwa miaka minne lakini Mourinho anaamini taratibu nyota huyo atarejea katika ubora wake. Akihojiwa Mourinho amesema Pogba anahitaji muda ili kuonyesha ubora wake kwani anafahamu soka la Italia, timu za kule zinacheza soka tofauti na Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment