Thursday, October 20, 2016

PIQUE KUKAA NJE WIKI TATU.

BEKI wa Barcelona, Gerard Pique anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa wiki tatu kufuatia majeruhi ya kifundo cha mguu aliyopata katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Manchester City jana huko Camp Nou. Mara ya kwanza ilionekana kuwa beki huyo anaweza kukaa nje kwa siku 10 lakini baada ya vipimo sasa imebainika kuwa itakuwa wiki tatu. Kutokana na hilo sasa Pique anatarajiwa kukosa mechi za La Liga dhidi ya Valencia, Granada na Sevilla pamoja na ule wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya City. Kwa upande mwingine beki wa kushoto Jordi Alba naye anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa wiki mbili kufuatia kupata majeruhi ya msuli wa paja katika mchezo huohuo wa jana.

No comments:

Post a Comment