Thursday, October 20, 2016

RODGERS AMTETEA TOURE.

MENEJA wa Celtic, Brendan Rodgers amesema hakuna yeyote duniani aliyeumia zaidi kuliko Kolo Toure baada ya kufungwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Monchengladbach. Beki huyo mkongwe wa kimataifa wa Ivory Coast makosa yake aliyofanya katika safu ya ulinzi ndio yalipelekea Lars Stindl na Andre Hahn kufunga mabao hayo mawili na kuipa timu hiyo ya Ujerumani ushindi wake wa kwanza katika hatua ya makundi. Toure mwenye umri wa miaka 35, naye pia anajilaumu kwa kipigo hicho. Akihojiwa, Rodgers amesema Toure ni mchezaji mkweli hivyo matukio ya jana lazima yamuumize. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa anamwamini Toure kama mpambanaji hivyo anadhani atasahau magumu hayo na kuendelea kucheza kwa ubora wake.

No comments:

Post a Comment