Thursday, October 20, 2016

SIWEZI KUBADILI FALSAFA ZANGU - GUARDIOLA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema kamwe hawezi kubadili falsafa yake pamoja na kikosi chake kufumuliwa mabao 4-0 na klabu yake ya zamani wa Barcelona. Lionel Messi alifunga hat-trick dhidi ya City huku kipa Claudio Bravo akitolewa kwa kushika mpira nje ya eneo lake. Akihojiwa Guardiola amesema hakuna mabadiliko atakayofanya na ataendelea kutumia falsafa hiyohiyo. Akizungumza kuhusu Bravo, Guardiola amesema ni kipa mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka kumi hivyo hana shaka naye pamoja na kosa alilofanya. Barcelona wanaongoza kundi C wakiwa na alama tisa, tano zaidi ya City.

No comments:

Post a Comment