Thursday, October 20, 2016

NINGEKUWA MAN UNITED KAMA FERGUSON ANGEKUWEPO - VAN PERSIE.

MSHAMBULIAJI nyota wa Fenerbahce Robin van Persie amesema angeweza kuwepo katika kikosi cha Manchester United katika mchezo wa leo wa Europa League kama Sir Alex Ferguson angekuwa bado yupo Old Trafford. Van Persie alichaguliw akuwa mchezaji bora wa mwaka wa United katika msimu wake wa kwanza Old Trafford 2012-2013 ambapo pia walitwaa taji la Ligi Kuu. Akihojiwa kama anadhani angeweza bado kuwa United ikiwa Ferguson angeendelea kubakia, Van Persie amesema anadhani bado angekuwa yuko United. Van Persie aliendelea kudai kuwa wakati akisajiliwa United kulikuwa na mipango ya Ferguson kubakia kwa miaka michache zaidi lakini hilo halikutokea.

No comments:

Post a Comment