Thursday, October 20, 2016

SIMEONE AVIMBA KICHWA NA KIKOSI CHAKE.

MENEJA wa Atletico Madrid, Diego Simeone amesema amefurahishwa na jinsi timu yake ilivyomiliki mchezo katika ushindi waliopata katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Rostov jana. Ushindi huo umeifanya Atletico kuongoza kundi D na Simeone amewapongeza wachezaji wake kwa mchezo mzuri. Simeone amesema ulikuwa mchezo mgumu lakini waliwafahamu wapinzani wao na jinsi wanavyocheza. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa wapinzani wao walikuwa wakijilinda kwa kipindi kirefu lakini hilo halikuwakatisha tama wachezaji wake kutengeneza nafasi chache na kutumia waliyopata na kuondoka na alama zote tatu.

No comments:

Post a Comment