Thursday, October 20, 2016

MICHO AJITUTUMUA PAMOJA NA UGANDA KUPANGWA KUNDI LA KIFO AFCON.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uganda, Milutin Sredojevic maarufu kama Micho, amesema kuwa hakuna kinachoshindikana baada ya kupangwa kundi moja na Ghana, Mali na Misri katika ratiba ya michuano ya Mataifa ya Afrika iliyopangwa jijini Libreville, Gabon jana jioni. Akihojiwa mara baada ya upangwaji wa ratiba hiyo, Micho alieleza kuwa wakipata maandalizi mazuri wana uwezo wa kupata matokeo mazuri dhidi ya timu kubwa walizonazo katika kundi D. Micho amesema siku zote hakuna linaloshindikana na ili uwe bora ni lazima upambane na walio bora ili kuonyesha uwezo wako. Kocha huyo alienndelea kudai kuwa kundi lao ni gumu na lenye ushindani lakini anawaamini wachezaji wake pamoja na uongozi wa Shirikisho la Soka la nchini hiyo-FUFA. Uganda wataanza kampeni zao za Afcon kwa kucheza na Ghana Januari 17, Misri Januari 21 mechi zote zikifanyika huko Port Gentil kabla ya kuivaa Mali katika mchezo wao wa mwisho wa kundi Januari 25 huko Oyen.

No comments:

Post a Comment