Wednesday, October 19, 2016

MAN UNITED IMEONGEZA MASHABIKI MILIONI NANE.

WINGA wa zamani wa Manchester United, Jasper Blomqvist anaamini klabu hiyo imejiongezea mashabiki milioni nane wa Paris Saint-Germain-PSG kufuatia kumsajili Zlatan Ibrahimovic majira ya kiangazi. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Sweden alicheza kwa miaka minne Parc des Princes, akishinda mataji 11 na klabu hiyo kabla ya kuondoka kiangazi kufuatia kumaliza mkataba wake. Akihojiwa Blomgvist amesema kutokana na umaarufu mkubwa wa Ibrahimovic nchini Sweden anadhani PSG watakuwa wamepoteza mashabiki wengi nchini humo wanaoweza kufikia hata milioni nane. Mkongwe huyo aliendelea kudai kuwa Ibrahimovic ana jina kubwa Sweden yuko kila mahali hata mpaka kipindi hiki ambacho ameacha kucheza soka.

No comments:

Post a Comment