Friday, October 21, 2016

KOMPANY, AGUERO BADO WANA NAFASI CITY - GUARDIOLA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema mshambuliaji Sergio Aguero na beki Vincent Kompany wote wana uhakika wa kazi yao katika klabu hiyo. Nyota wote wawili hawakuanza katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelona juzi, huku Kompany akiwa hakuonekana hata katika benchi la wachezaji wa akiba na kufanya kuzuka kwa tetesi kuwa hawako katika mipango ya kocha huyo. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Guardiola amesema Kompany yuko fiti sasa na kuhusu Aguero alimuacha katika mchezo wa juzi kwasababu za kiufundi. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kama Aguero akiamua kuondoka itakuwa ni uamuzi wake mwenyewe. Guardiola alithibitisha Pablo Zabaleta na Bacary Sagna kuwa wote wanatarajia kukosa mchezo wa Ligi Kuu wa Jumapili hii dhidi ya Southampton kwasababu ya majeruhi.

No comments:

Post a Comment