Tuesday, October 18, 2016

MOURINHO AIPONDA LIVERPOOL KUFUATIA SARE.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema Liverpool sio timu ya kwanza ya ajabu kama inavyoripotiwa na vyombo vya habari, baada ya timu hizo kutoka sare ya bila kufungana jana. Katika mchezo huo wa Anfield uliokuwa na nafasi chache, wenyeji Liverpool walionyesha kutawala mchezo huo kwa kiasi kikubwa kufuatia wapianzani wao muda mwingi kucheza kwa kujihami. Akihojiwa Mourinho amesema jambo la muhimu ni kuwa wamepata alama moja ambayo imewazuia wapinzani wao kupata alama tatu. Kwa upande wa meneja wa Liverpool Jurgen Klopp, yeye ameonyesha kutofurahishwa na kikosi chake kwani walikuwa wakitaka kucheza haraka na kupoteza umakini katika pasi zao. Matokeo hayo ynaiacha Liverpool katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu wakiwa na alama saba huku United wakiwa nyuma yao kwa tofauti ya alama tatu kwenye nafasi ya saba.

No comments:

Post a Comment