Wednesday, October 19, 2016

SANCHEZ, OZIL WAMNYIMA USINGIZI WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger anaamini ushindano wao wa mataji unaweza kuwasaidia kuwashawishi winga Alexis Sanchez na kiungo Mesut Ozil kusaini mikataba mipya ya muda mrefu na klabu hiyo. Ozil na Sanchez wameingia katika miezi 20 ya mwisho katika mikataba yao ya sasa kwenye klabu hiyo na wanatarajiwa kusaini mikataba mipya minono ambayo itawafanya kubakia Emirates zaidi ya 2018. Wenger amekiri kuwa wakati majadiliano kuhusu masuala ya fedha yakiwa jambo muhimu, maendeleo ya timu uwanjani yanaweza kuchukua nafasi kubwa. Meneja huyo amesema wachezaji kama Sanchez na Ozil huwa hawaangalii sana masuala ya kifedha kwasababu tayari ni matajiri, hivyo jambo la muhimu litakuwa na maendeleo ya timu na jinsi inavyoshindania mataji. Arsenal kwasasa wanaongoza msimamo wa kundi lao katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na wanatarajiwa kucheza na wakaribisha Ludogorets Razgrad ya Bulgaria leo.

No comments:

Post a Comment