Friday, November 18, 2016

AC MILAN YAMLENGA STURRIDGE JANUARI.

KLABU ya AC Milan, inadaiwa kujipanga kumuwania mshambuliaji wa Liverpool, Daniel Sturridge Januari mwakani. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27, amekuwa akishindwa kupata nafasi katika kikosi cha meneja Jurgen Klopp. Lakini uwezo mkubwa alionao mchezaji huyo unadaiwa kumvutia meneja wa Milan Vincenzo Montella ambaye anaweza kutoa ofa ya paundi milioni 30 ili kumnasa. Hata hivyo, uhamisho huo unadaiwa kuwa utategemea kuondoka kwa Carlos Bacca.

No comments:

Post a Comment