Friday, November 18, 2016

GUARDIOLA AMUWANIA BEKI WA BENFICA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola anataka kuimarisha zaidi safu yake ya ulinzi kwa kumuania beki wa kushoto wa Benfica Alex Grimaldo. Lakini meneja huyo anaweza kushindwa kunasa saini ya beki huyo kufuatia taarifa kuwa Benfica wanaweza kutaka paundi milioni 38.5. Guardiola amekuwa akimfahamu Grimilo kwa kipindi kirefu toka alipokuwa Barcelona. Hata hivyo, uhusiano wao huo haudhaniwi kama unaweza kuwa ushawishi wa kumng’oa nyota huyo nchini Ureno.

No comments:

Post a Comment