Wednesday, November 30, 2016

BARCELONA YAMUWANIA MKONGWE WA CROATIA.


KLABU ya Barcelona inadaiwa kukaribia kukamilisha usajili wa Darijo Srna kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu huu. Mabingwa Hispania wanataka kuimarisha safu yao ya ulinzi upande wa kulia lakini wanakabiliwa na ukata katika bajeti yao ya usajili wa dirisha dogo lakini Srna anaweza kuondoka Shakhtar Donetsk bure. Nyota huyo wa kimataifa wa Croatia alikuwa akitaka kuondoka Ukraine kipindi kirefu na mkurugenzi wa ufundi wa Barcelona Robert Fernandez amekuwa akifanya naye mawasiliano. Barcelona wanaweza kusajili kumsajili mchezaji ghali kama wakiuza mchezaji huku Aleix Vidal akiwa mchezaji pekee ambaye anaweza kuwapatia fedha hizo wanazohitaji.

No comments:

Post a Comment