Tuesday, November 22, 2016

BAYERN KUMKOSA NEUER KESHO.

KIPA wa Bayern Munich, Manuel Neuer anatarajia kuukosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kesho watakaocheza dhidi ya Rostov nchini Urusi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 amepata majeruhi ambayo yatamlazimu kubakia Munich kwa ajili ya matibabu huku Tom Starke na Sven Ulreich mmojawapo akitarajiwa kuchukua nafasi yake. Bayern ambao walitandikwa bao 1-0 na Borussia Dortmund katika mchezo wa Bundesliga Jumamosi iliyopita, tayari wameshafuzu hatua ya 16 bora ya michuano hiyo na wanashikilia nafasi ya pili katika kundi D wakiwa na alama tisa baada ya kucheza michezo minne. Atletico Madrid ya Hispania ndio wanaoongoza kundi hilo kwa kuwa na alama 12 wakati Rostov na PSV Eindhoven ya Uholanzi wao wakiwa na alama moja kila mmoja huku kukiwa kumebaki michezo miwili.

No comments:

Post a Comment