Tuesday, November 22, 2016

MASHABIKI WA SEVILLA NA JUVENTUS WAPIGANA.

MASHABIKI wa Juventus na Sevilla jana usiku wamepigana na kupeleka shabiki mmoja Muitaliano kuumia vibaya baada ya kuchomwa kisu na wengine watatu kuumia. Taarifa kutoka nchini Hispania zinadai kuwa kundi la watu wapatao 30 lilikwenda katika bar moja iliyoko kituo cha kihistoria cha jiji hilo la Sevilla ambapo kulikuwa na mashabiki wa Juventus. Picha za video zimeonyesha ugomvi mkubwa ukizuka miongoni mwa mashabiki hao ikiwemo shabiki mmoja akirusha kiti baada ya kutoka nje ya bar hiyo kabla ya polisi hawajaingilia kati na kuwatuliza. Sevilla na Juventus zinatarajiwa kukwaana katika Uwanja wa Ramon Sanchez Pizjuan baadae leo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment