Wednesday, November 30, 2016

BOSI WA PIRELLI ATAKA KUMPELEKA MESSI INTER MILAN.

MWENYEKITI wa kampuni ya Kutengeneza matairi ya Pirelli, Marco Tronchetti Provera ambao ndio wadhamini wakubwa wa Inter Milan amesema bado ana matumaini ataweza kutimiza ndoto za kumleta Lionel Messi katika klabu hiyo kutoka Barcelona. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina kwa mara nyingine mustakabli wake umeleta mjadala mkubwa katika wiki za karibuni huku kukiwa na tetesi kuwa mazungumzo hayaendi kama yalivyotarajiwa Camp Nou. Taarifa zinadai kuwa mkurugenzi wa michezo wa Paris Saint-Germain-PSG Patrick Kluivert ameshazungumza na baba yake ya Messi kujadili uwezekano wa nyota huyo kwenda kwa mabingwa hao wa Ligue 1. Pamoja na hayo, Messi mwenyewe mara zote amekuwa akisisitiza kuwa anatarajiwa kurejea katika klabu yake ya utotoni ya Newell’s Old Boys ya Argentina wakati muda wake Barcelona utakapomalizika. Provera amesema lengo lake ni kumshawishi nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 kufikiria kuichezea Inter.

No comments:

Post a Comment