Monday, November 21, 2016

CONTE AMMWAGIA MISIFA COSTA.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amemuhabalisha Diego Costa kuendelea kufanya anayofanya baada ya kuipeleka Chelsea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu. Bao pekee alilofunga Costa katika mchezo huo dhidi ya Middlesbrough uliofanyika katika Uwanja wa Riverside lilitosha kuipa Chelsea ushindi wake wa sita mfululizo katika ligi na kuzipita Liverpool na Manchester City. Nyota huyo kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 28, hilo linakuwa bao lake la 10 msimu huu. Akihojiwa Conte amesema Costa ni mmoja wa washambuliaji bora duniani na anadhani amewaonyesha kwa vitendo wale wote waliokuwa wakimkosoa na kuhoji uwezo wake.

No comments:

Post a Comment