Monday, November 21, 2016

ROMA, GALATASARAY WAMUWANIA DEBUCHY.

KLABU za AS Roma na Galatasaray zinadaiwa kumuwania beki wa Arsenal, Mathieu Debuchy ambaye anaonekana kutokuwa na nafasi katika klabu hiyo. Beki huyo mwenye umri wa miaka 31, amecheza mechi mbili pekee za Ligi Kuu katika misimu miwili iliyopita katika kikosi cha Arsene Wenger, kufuatia kupelekwa kwa mkopo katika Bordeaux Januari mwaka huu. Hata hivyo, anaweza kupewa nafasi ya kurejea katika kikosi cha kwanza huku Roma na Galatasaray zote zikidaiwa kumuwania nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa. Debuchy alirejea kutoka katika majeruhi kwa kufunga bao katika mchezo wa kikosi cha wachezaji chini ya miaka 23 na anaweza kurejeshwa katika mipango ya Wenger kufuatia kuumia kwa Hector Bellerin.

No comments:

Post a Comment