Wednesday, November 23, 2016

IBRAHIMOVIC KUPEWA MSIMU MMOJA ZAIDI UNITED.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amethibitisha kuwa Zlatan Ibrahimovic ataendelea kubakia katika klabu hiyo kwa ajili ya msimu wa 2017-2018. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Mourinho amesema wanafurahia kuwa na Ibrahimovic hivyo wana mpango wa kumuongeza msimu mwingine wa pili. Mourinho aliendelea kudai kuwa baada ya miaka miwili anaweza kufanya anachotaka kwasababu atakuwa huru ila kwasasa bado wataendelea kuwa naye. Ibrahimovic alisajiliwa United kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Paris Saint-Germain huku kukiwa na kipengele cha kuongezewa mwaka mwingine.

No comments:

Post a Comment