Wednesday, November 23, 2016

PICHA ZA VIDEO ZAMUWEKA MATATANI DRINKWATER.

KIUNGO wa Leicester City, Danny Drinkwater ameshitakiwa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa tuhuma za kumpiga kiwiko mchezaji wa Watford Valon Behrami. Tukio hilo lilitokea wakati wa kipindi cha pili cha mchezo wa Ligi Kuu ambao Leicester walichapwa mabao 2-1 Jumamosi iliyopita, lakini mwamuzi wa mchezo huo hakuling’amua tukio hilo. Drinkwater amepewa muda mpaka leo usiku awe amejibu tuhuma za tukio hilo ambalo lilichunguzwa na jopo la waamuzi kupitia picha za video. Jopo la waamuzi hao kila mmoja atapata nafasi ya kulitizama tukio kwa makini kabla ya kuamua kutoa uamuzi wao.

No comments:

Post a Comment