Tuesday, November 22, 2016

JUSTIN BIEBER AVAMIA MAZOEZI YA BARCELONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Celtic kesho kufuatia kurejea mazoezini baada ya kuugua. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina amefanikiwa kupona maradhi yaliyomlazimu kushindwa kucheza mchezo wa La Liga dhidi ya Malaga Jumamosi iliyopita. Lakini mapema jana Messi alifanya mazoezi na wenzake ambako waliungana na mwanamuziki wa mashuhuri duniani wa muziki wa pop Justin Bieber. Barcelona wanaongoza kundi C kwa tofauti ya alama mbili dhidi ya Manchester City na wanahitaji ushindi katika mchezo wao wa kesho ili kujihakikishia nafasi ya kutinga hatua ya timu 16 bora.

No comments:

Post a Comment