Thursday, November 17, 2016

MOURINHO AMTAKA DEMBELE.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho anadaiwa kutaka kumleta nyota wa Celtic Moussa Dembele kwani anadhani anaweza kuwa Didier Drogba ajaye. Taarifa zinadai kuwa Mourinho amekuwa akimfuatilia chipukizi huyo mara tatu msimu uliopita kabla hajaondoka Fulham na kwenda Celtic. Hata hivyo, Celtic wanadaiwa kuwa hawataweza kumuachia Dembele, ambaye amefunga mabao matatu katika mechi nne za Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu, katika kipindi cha usajili wa Januari. Manchester City, Arsenal, Chelsea na Bayern Munich zote pia zinadaiwa kumfuatilia nyota huyo mwenye umri wa miaka 20, wakati Tottenham Hotspurs walishindwa kumsajili Januari mwaka huu.

No comments:

Post a Comment