Wednesday, November 23, 2016

POCHETTINHO AWATUPIA LAWAMA WACHEZAJI WAKE.


MENEJA wa Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino amedai kuwa wachezaji wake walikosa ubora uliohitajika ili kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Kipigo cha mabao 2-1 walichopata kutoka kwa Monaco kilitosha kuwaengua katika michuano hiyo. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Pochettino amesema wanahitaji kuimarika zaidi kiakili na kuwa tayari kwa kila mechi. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kutokea mwanzoni mwa msimu alisema changamoto yao kubwa sio nguvu bali ni ufundi wa kuweza kuziweka akili tayari kucheza Jumamosi na baadae Jumanne au Jumatano.

No comments:

Post a Comment