Monday, November 21, 2016

SPURS YAMGEUKIA TENA SANDRO BAADA YA JANSSEN KUSHINDWA KUNG'AA.

KLABU ya Tottenham Hotspurs inatarajiwa kwa mara nyingine kutupa ndoano kumuwania mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, Sandro katika usajili wa dirisha dogo Januari mwakani. Spurs walikuwa wameonyesha nia ya kumsajili wakati wa kiangazi lakini waliamua kumchukua Vincent Janssen badala yake huku Sandro mwenyewe akichagua kubakia Malaga ambako alisaini mkataba wa miaka mitatu. Hata hivyo, Spurs wameanza tena kumuwania nyota huyo kufuatia Janssen kushindwa kung’ara vyema katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo. Sandro mpaka sasa ameshafunga mabao matano katika mechi 10 alizoichezea Malaga toka kuanza kwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment