Tuesday, December 20, 2016

AC MILAN YAMNYATIA FELLAINI.

KIUNGO Marouane Fellaini anaweza kupewa nafasi ya kuondoka Manchester United Januari wakani na AC Milan. Milan wamekuwa wakihusishwa na tetesi za kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji katika kipindi cha majira ya kiangazi lakini akaendelea kubakia Old Trafford na kuwa sehemu ya mipango ya meneja Jose Mourinho. Hata hivyo, hivi karibuni amekuwa akikosolewa vikali na mashabiki wa klabu hiyo haswa pale aliposababisha penati ambayo iliwapa nafasi Everton kutoa sare ya bao 1-1 kule Goodison park. Kutokana na hilo uhamisho wa Fellaini katika kipindi cha Januari unaonekana unaweza kufanyika na Milan wanataka kutumia mwanya huo kumnasa.

No comments:

Post a Comment