Tuesday, December 20, 2016

GUARDIOLA NA MOURINHO KUKUTANA MAREKANI KIANGAZI.

MCHEZO wa kwanza wa derby ya Manchester kuchezwa nje ya Uingereza huenda ukafanyika nchini Marekani katika kipindi cha majira ya kiangazi. Manchester City inayonolewa na Pep Guardiola na Manchester United iliyokuwa chini ya Jose Mourinho ilikuwa wakutane jijini Beijing, China Julai mwaka huu. Hata hivyo, mvua kubwa iliyonyesha katika jiji hilo ilipelekea Uwanja wa Bird Nest kushindw akuchezeka hivyo mchezo baina timu hizo kuahirishwa saa sita kabla. Timu zote hizo zinatarajiwa kusafiri kwenda nchini Marekani Julai mwakani kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2017-2018. Ingawa hakuna maelezo yeyote yaliyotolewa, timu hizo zinatarajiwa kushiriki katika michuano ya Ubingwa wa Kimataifa hatua ambayo inaweza kuwakutanisha.

No comments:

Post a Comment