Tuesday, December 20, 2016

SUPER FALCON WAMALIZA MGOMO BAADA YA KUPEWA CHAO.

TIMU ya taifa ya soka ya wanawake ya Nigeria, hatimaye wamemaliza maandamano yao ya kugoma kutoka hotelini jijini Abuja baada ya kulipwa fedha walizokuwa wakidai. Timu hiyo ilikuwa ikidai kiasi cha dola 23,650 kwa kila mchezaji kutoka Shirikisho la Soka la Nigeria kufuatia ushindi wao waliopata wa taji la Mataifa ya Afrika. Kikosi hicho kinachojulikana kama Super Falcon kimekuwa hotelini hapo toka Desemba 6 mwaka huu pindi walipotua kutoka katika michuano hiyo. Taarifa kutoka kwa msemaji wa timu imedai kuwa wachezaji wote wameshaondoka hotelini baada ya kupewa stahiki zao. Nigeria imetwaa taji hilo la wanawake mara nane kati ya 10 toka michuano hiyo ilipoanzishwa mwaka 1998.

No comments:

Post a Comment