Tuesday, December 20, 2016

MADRID WAPUNGUZIWA ADHABU.


KLABU ya Real Madrid imetangaza kuwa adhabu yao ya kufungiwa kusajili katika vipindi viwili imepunguzwa mpaka kipindi kimoja na Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS. Madrid sambamba na majirani zao Atletico Madrid walilimwa adhabu hiyo Januari mwaka huu baada ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuwakuta na hatia ya kukiuka sheria za usajili kwa wachezaji wa kimataifa walio umri chini ya miaka 18. Mabingwa wa Hispania Barcelona nao pia walikutwa na adhabu kama hiyo mwaka 2014. Rufani yao FIFA ilitupiliwa mbali SEptemba mwaka huu hatua ambayo iliwafanya Madrid kwenda CAS. Kufuatia maamuzi hayo mapya sasa Madrid wataweza kuendelea kusajili wachezaji wapya msihoni mwa msimu huu pindi watakapomaliza kutumikia adhabu hiyo Januari mwakani.

No comments:

Post a Comment