Tuesday, December 20, 2016

BOATENG NJE WIKI SITA.

BEKI wa Bayern Munich, Jerome Boateng anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi wiki sita baada ya kufanyiwa upasuaji wa bega. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani hakuwepo katika mchezo ambao Bayern walifungw amabao 3-2 na Rostov kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Novemba 23 na alifanyiwa upasuaji mapema leo. Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, upasuaji wa Boateng ulikwenda salama na sasa anatarajiwa kurejea uwanjani mapema mwezi Februari mwakani. Msimu huu Boateng umekuwa sio mzuri sana kwake kwnai amekuwa akiandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment