Tuesday, December 20, 2016

ARSENAL KUMFUATA REUS KAMA SANCHEZ NA OZIL WAKIGOMA.

KLABU ya Arsenal inadaiwa bado kuendelea kumuweka katika rada zake Marco Reus kama Alexis Sanchez au Mesut Ozil mmoja wapo akliamua kuondoka Emirates. Nyota huyo wa kimataiaf wa Ujerumani kwa kipindi kirefu amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia Ligi Kuu lakini bado ameendelea kuwa mwaminifu kwa klabu yake ya Borussia Dortmund. Reus ana mkataba na Dortmund unaomalizika mwaka 2019 lakini anaweza kupewa ofa ya fedha nyingi kama Arsene Wenger akishindwa kuwazuia wachezaji wake muhimu. Sanchez na Ozil wako katika mazungumzo ya kuongezwa mkataba Arsenal lakini hakuna yeyote ambaye mpaka sasa ameshakubali dili jipya hivyo kuzuka tetesi kuwa wanaweza kuondoka.

No comments:

Post a Comment