Tuesday, December 20, 2016

MESSI HAENDI KOKOTE - BARTOMEU.

RAIS wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amedai Lionel Messi ana uhakika wa kuendelea kubakia klabuni hapo, pamoja na kwamba mazungumzo ya mkataba mpya bado hayajafanyika. Mustakabali wa Messi umekuwa mjadala kipindi hiki kufuatia kuingia miezi 18 ya mwisho katika mkataba wake unaotarajiwa kuisha Juni mwaka 2018. Makamu wa rais wa klabu hiyo, Jordi Mestre alibainisha Jumapili iliyopita kuwa Barcelona bado hawajaanza mazungumzo na nyota huyo, ingawa bado wana matumaini yakuendelea kuwa naye. Akihojiwa mapema leo, Bartomeu alithibitisha kauli ya Mestre kuwa bado hawajaanza mazungumzo na Messi lakini wana uhakika mchezaji mwenyewe bado anapenda kuitumikia klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment