Wednesday, December 21, 2016

LIVERPOOL ITAKUWA SHWARI BILA MIMI - MANE.

MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Sadio Mane ana uhakika klabu hiyo inaweza kuendelea vyema bila uwepo wake wakati atakapoondoka kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika mwezi ujao. Mane ambaye anaongoza orodha ya wafungaji katika klabu hiyo akiwa na mabao nane amebakisha mechi tatu pekee za Ligi Kuu dhidi ya Stoke City, Manchester City na Sunderland kabla ya hajakwenda kujiunga na timu yake ya taifa ya Senegal. Nyota huyo anatarajiwa kuwa na Senegal mpaka hatua ya mwisho ambayo nchi hiyo itafikia kabla ya kurejea tena Uingereza kuitumikia Liverpool. Akihojiwa Mane amesema sio jambo rahisi kuondoka na kuwaacha wachezaji wenzake wa Liverpool wakipigana peke yao lakini hana jinsi kwani lazima akalitumikie taifa lake kwani ni moja ya ndoto zake pia. Mane aliendelea kudai kuwa anaamini kikosi chao kiko vizuri na wanaweza kuendelea vyema hata bila uwepo wake.

No comments:

Post a Comment