Friday, December 23, 2016

ADHABU YA FIFA YAMTESA EBOUE.

BEKI wa kimataifa wa Ivory Coast, Emmanuel Eboue amekiri kuwa anapata tabu kuzoea adhabu ya kufungiwa kutocheza soka kwa mwaka mzima mpaka muda mwingine anafikiria kujiua. Nyota huyo alifungiwa mwaka mmoja na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA ikiwa kama sehemu ya adhabu kwa kushindwa kulipa deni alilokuwa akidaiwa na wakala wake wa zamani Sebastian Boisseau. Mkataba wa Eboue na Sunderland ulisitishwa baada ya FIFA kutoa adhabu hiyo, kufuatia madai ya Boisseau kudai kitita cha karibu paundi milioni moja ikiwa ni sehemu ya stahiki yake aliyotakiwa kupewa baada ya kufanikisha uhamisho wake kwenda Galatasaray kutoka Arsenal mwaka 2011. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 amekuwa akifanya mazoezi na timu za chini jijini London ili aendelee kuwa fiti lakini amebainisha kuwa adhabu hiyo inamtesa sana. Akihojiwa Eboue amesema kuna baadhi ya siku huwa hajisikii kabisa kutoka kitandani na kuna wakati alifikiria hata kujiua lakini anashukuru kwani familia inamtia moyo na kumpa nguvu za kuendelea.

No comments:

Post a Comment