Friday, December 23, 2016

OSCAR ATIMKIA CHINA RASMI.

KLABU ya Chelsea na Shanghai SIPG zimekubaliana uhamisho wa kiungo Oscar kwenda Ligi Kuu ya China katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi Januari mwakani. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 25 mapema mwezi huu alibainisha kuwa uhamisho wake ulikuwa umekamilika kwa asilimia 90. Oscar alijiunga na Chelsea akitokea Internacional kwa kitita cha paundi milioni 25 mwaka 2012 na kufunga mabao 38 katika mechi 203 alizoichezea klabu hiyo. Katika taarifa yake ilitolewa mapema leo Chelsea walithibitisha taarifa hizo kuwa kiungo huyo atakwenda nchini China Januari mwakani. Oscar ambaye amekuwa akihangaika kupata nafasi chini ya meneja mpya Antonio Conte, anakwenda Shanghai kujiunga na meneja wa zamani wa Chelsea Andre Villas-Boas.

No comments:

Post a Comment