Wednesday, December 21, 2016

KOCHA CAMEROON ATAKA WACHEZAJI WALIOGOMA KUCHUKULIWA HATUA.

BEKI wa Liverpool Joel Matip ni mmoja kati ya wachezaji saba ambao wamesema hawataki kwenda kushiriki michuano ya Mataifa ya Afrika ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 14 mwakani. Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka la nchi hiyo-FECAFOOT imedai kuwa beki huyo ametoa kauli hiyo kupitia uzoefu wake aliopata katika benchi la ufundi lililopita. Beki wa West Browich Albion, Allan Nyom ni miongoni mwa orodha ya wachezaji saba waliogoma. FECAFOOT inaweza kuliagiza Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuwasimamisha wachezaji hao kuzitumikia klabu zao kwa kipindi cha wiki tatu michuano hiyo itakapokuwa ikiendelea. Kocha wa Cameroon, Hugo Broos amesema wachezaji hao waliogoma wameweka maslahi yao mbele kuliko yale ya timu ya taifa na shirikisho lina haki ya kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za FIFA. WEngine waliopo katika mgomo huo ni pamoja na Andre Onana wa Ajax Amsterdam, Guy N’dy Assembe wa Nancy, Maxime Poundeje wa Bordeaux, Andre-Frank Zambo Anguissa wa Marseille na Ibrahim Amadou wa Lille. Cameroon imepangwa kundi A sambamba na wenyeji Gabon, Burkina Faso na Guinea Bissau.

No comments:

Post a Comment