Wednesday, December 21, 2016

UNITED KUMUONGEZA MKATABA MOURINHO.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kujipanga kumpa ofa ya kumuongeza mkataba meneja wake Jose Mourinho nyuma ya mkataba wake wa sasa wa miaka mitatu. Wamiliki wa United wanadaiwa kuridhishwa na kazi aliyofanya Mourinho toka alipotua Old Trafford ana wanaamini anaweza kufanikisha wakatwaa taji la 21 la Ligi Kuu kwa klabu hiyo. Pamoja na United kuanza msimu kwa kusuasua lakini meneja huyo amefanikiwa kuirejeshea makali yake kwa kushinda mechi tatu mfululizo ambazo kwa kiasi kikubwa zimewasaidia kupunguza pengo la alama baina yake na timu zilizokuwa katika orodha nne za juu. Inafahamika kuwa mustakabali wa Mourinho mwenye umri wa miaka 53 unategemea matokeo na aina ya uchezaji lakini familia ya Glazers imeonyesha kufurahishwa na anachokifanya meneja huyo mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment