Wednesday, December 21, 2016

ARSENAL YAJIANDAA KUTUPIA NDOANO KWA KINDA LA VALENCIA.

KLABU ya Arsenal inadaiwa kujipanga kumuwania beki wa kushoto wa Valencia, Jose Gaya. Gaya anaonekana kama mmoja ya wachezaji wanaoibuka kwa kasi Ulaya na kuna kila dalili kuwa Valencia hataweza kumzuia chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 21 kuondoka. Manchester United na Chelsea nazo pia zimetajwa kumuwania chipukizi huyo lakini Arsenal ndio wanaoonekana kumuhitaji zaidi ili kuimarisha eneo lao la ulinzi la kushoto. Katika taarifa nyingine kutoka ndani ya klabu hiyo imedaiowa kuwa Wenger ameonyesha dalili kuwa ataendelea kuinoa klabu hiyo kupita mkataba wake wa sasa.

No comments:

Post a Comment