Wednesday, December 21, 2016

WEST HAM WAMNYATIA RASHFORD.

KLABU ya West Ham United inadaiwa kujiandaa kuwawania kwa mkopo nyota wa Manchester United Marcus Rashford na Anthony Martial katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo. West Hama kwasasa wako juu kidogo la eneo la kushuka la kushuka daraja katika msimamo wa Ligi Kuu na wanataka kuongeza nguvu katika safu yao ya ushambuliaji na washambuliaji hao wa United wanaweza kuleta tofauti ili waweze kuepuka kushuka daraja. Mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi ndio alikuwa chaguo namba moja la West Ham lakini meneja Slaven Bilic ameamua kuangalia uwezekano mwingine kwasababu Chelsea inaweza ikashindwa kumruhusu kuondoka januari. Kutokana na Rashford na Martial kupoteza nafasi zao katika kikosi cha kwanza United msimu huu, West Ham wana matumaini kuwa wakiwaahidi muda zaidi wa kucheza inaweza kuwarahisishia kuwapata.

No comments:

Post a Comment