Friday, December 23, 2016

CHELSEA INAWEZA KUPAMBANA NA SHINIKIZO - CONTE.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amesema klabu hiyo imevuka mategemeo msimu huu lakini ana uhakika kikosi chake kitatumia uzoefu wao ili kuepuka shinikizo la kuwepo kileleni mwa msimo wa Ligi Kuu. Baada ya kuanza kwa kusuasua, Chelsea ambao walimaliza nafasi ya 10 msimu uliopita, wamekwenda kushinda mechi 11 mfululizo za ligi ushindi ambao umewasaidia kutengeneza pengo la alama sita kileleni baada ya kucheza mechi 17. Akihojiwa Conte amesema hakuna mtu yeyote aliyefahamu kuwa Chelsea itakuwa kileleni mwa msimamo wa ligi. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa anadhani wamepata uwiano sahihi na kipindi ambacho wamebakisha mechi mbili kabla ya kuingia duru la pili ni muhimu kwa wachezaji wake kuendelea kutumia uzoefu wao kuzuia shinikizo. Chelsea wanatarajiwa kukutana na Bournemouthkatika Uwanja wa Stamford Bridge Jumatatu ijayo.

No comments:

Post a Comment