Friday, December 23, 2016

DRAXLER NJIANI KWENDA PSG.

KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG inadaiwa kufikia makubaliano na VfL Wolfsburg kwa ajili ya uhamisho wa Julian Draxler. Tetesi zimekuwa zikizagaa kwa wiki kadhaa kuwa PSG wanamtaka nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani na taarifa za mapema wiki hii kutoka Ufaransa zimedai mmiliki wa klabu hiyo anataka kutoa ofa huku mchezaji mwenyewe akiridhia kuondoka. Draxler mwenye umri wa miaka 23 anadaiwa kuwa tayari ameshazungumza na mkurugenzi wa michezo wa PSG Patrick Kluivert na kilichobakia ni hatua za mwisho za kukamilisha uhamisho wake na kupewa mkataba unaokadiriwa utakuwa wa miaka mitatu au minne na nusu. Draxler alianza kucheza soka lake katika klabu ya Schalke akikaa hapo kwa kipindi cha miaka minne kabla ya kutimkia Wolfsburg.

No comments:

Post a Comment