Friday, December 23, 2016

RAIS WA BOCA JUNIORS ATHIBITISHA SAFARI YA TEVEZ CHINA.

RAIS wa Boca Juniors, Daniel Angelici amedokeza kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kumpoteza mshambuliaji wao Carlos Tevez kufuatia taarifa za ofa kubwa aliyopewa kutoka China. Nyota huyo wa zamani wa Manchester United na Manchester City amepewa ofa inayokadiriwa kufikia kitita cha paundi 615,000 kwa wiki na klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki Ligi Kuu ya China. Akihojiwa Angelici amesema amekuwa na mahusiano ya karibu na Tevez na kwa jinsi hali inavyokwenda anadhani itakuwa vigumu kwa mshambuliaji huyo kubaki klabuni hapo. Rais huyo aliendelea kudai kuwa akiwa kama kiongozi na mshabiki wa klabu hiyo anataka Tevez abaki lakini ukitizama ofa kubwa aliyopewa kutoka China anadhani itakuwa ngumu kwa mshambuliaji huyo kuikataa. Tevez mwenye umri wa miaka 32, ana mkataba na Boca utakaomalizika Juni mwaka 2018 na anatarajiwa kusafiri kwenda China kukamilisha uhamisho wake mwezi ujao kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi ya huko Februari.

No comments:

Post a Comment