Friday, December 23, 2016

WEST BROM WATUMA OFA KWA SCHNEIDERLIN.

KLABU ya West Bromwich Albion imetenga ofa ya ya kiasi cha paundi milioni 13 kwa ajili ya Morgan Schneiderlin ambaye ataruhusiwa kuondoka Manchester United kama ikitolewa ofa sahihi. Meneja wa West Brom alithibitisha ofa hiyo, wakati meneja wa United Jose Mourinho akidai kuwa kama wakipata ofa nzuri hawezi kumzuia kiungo huyo kuondoka. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27, alijiunga na Southampton kwa kitita cha paundi milioni 25 Julai mwaka 2015 lakini amefanikiwa kucheza dakika 11 pekee msimu huu. Everton nao pia wanatajwa kumuwania kiungo huyo.

No comments:

Post a Comment