Wednesday, January 4, 2017

WACHEZAJI WANGU WALIGOMBA KUFUNGWA - WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kikosi chake kiligoma kupoteza mchezo kufuatia kutoka nyuma wakiwa wamefungwa mabao 3-0 na kutoa sare ya mabao 3-3 dhidi ya Bournemouth. Hiyo ni mara ya kwanza kwa Arsenal kufanikiwa kupata alama baada ya kufungwa mabao matatu katika mchezo wa Ligi Kuu. Akihojiwa Wenger amesema mchezo huo ulikuwa ni jaribio tosha la kimwili na kiakili, lakini mwishoni wamehuzunishwa kwa kutoshinda. Wenger aliendelea kudai kuwa walihitaji kushinda mchezo huo lakini haikuwa rahisi kwani timu kubwa zingine nazo zilipoteza mechi zao kwa Bournemouth ikiwemo Liverpool.

No comments:

Post a Comment