Wednesday, March 29, 2017

BARCELONA WASHTUSHWA NA ADHABU ALIYOPEWA MESSI.

KLABU ya Barcelona imetoa taarifa wakidai kushtushwa kwa adhabu ya kufungiwa mechi nne za kimataifa nyota wao Lionel Messi. Messi amelimwa adhabu hiyo kufuatia kumtolea maneno machfu mwamuzi wakati Argentina iliposhinda bao 1-0 katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Chile wiki iliyopita. Adhabu hiyo ilitangazwa saa chache kabla ya mchezo wao dhidi ya Bolivia jijini La Paz jana. Kukosekana kwa Messi kumepelekea Argentina kutandikwa mabao 2-0 na kuwafanya kushuka mpaka nafasi ya tano katika msimamo wa nchi za Amerika Kusini-CONMEBOL. Kaika taarifa yake Barcelona wamedai kushtushwa na taarifa hiyo ilitolewa na Kamati ya Nidhamu ya FIFA na kuona haikuwa haki na kuongeza kuwa wanamuunga mkono nyota wao kwenye kipindi hiki.

No comments:

Post a Comment