Friday, March 31, 2017

PSG KUWAKOSA MARQUINHOS NA KRYCHOWIAK.

BEKI wa kimataifa wa Brazil, Marquinhos na kiungo wa kimataifa wa Poland Grzegorz Krychowiak wanatarajiwa kukosa mchezo wa fainali ya Kombe la Ufaransa ambapo Paris Saint-Germain-PSG watacheza dhidi ya Monaco kesho. PSG walibainisha taarifa hizo mapema leo baada ya kutowajumuisha nyota hao katika orodha ya wachezaji watakaokuwepo kwenye mchezo huo utakaofanyika jijini Lyon. Marquinhos alitolewa wakati wa mapumziko katika ushindi wa mabao 3-0 waliopata Brazil dhidi ya Paraguay baada ya kuzumbuliwa na majeruhi ya nyonga. Krychowiak ambaye pia alikuwa kwenye majukumu ya kimataifa katikati ya wiki, naye aliondoka katika kambi ya Poland kufuatia kuumia mbavu.

No comments:

Post a Comment